Tigo
  • KRISTO TUMAINI LETU


    SWAHILI
     


    Hili ndilo neno kuu la Mkutano wa Injili wa hadhara ambao unafanyika viwanja vya Kanisa la Waadventista Wa-Sabato Ilala. 
    Mnenaji mkuu wa mkutano huu ni Mwinjilisti Yared Omolo. Kama Bwana alivyomtumia hapo kabla, atamtumia pia kwa majuma mawili tangu tarehe 18-31 Julai 2015. 
    Pia kutakuwa na masomo ya Afya yatakayotolewa na daktari kila siku ya mkutano. 
    Sambamba na hilo, kutakuwa na huduma ya upimaji wa afya za watu. 
    Karibu wewe, jirani, ndugu, jamaa na rafiki yako tubarikiwe sote kwa pamoja. 
    "KARIBU.. KARIBU.. KARIBU." 

     SABATO MAALUM YA KUMSHUKURU MUNGU KWA WEMA WAKE MWAKA 2014
    Sabato ya tarehe 20 Desemba 2014 ilikuwa ni siku maalum ya kumshukuru Mungu kwa wema na fadhili zake kwa mwaka 2014. Siku hii iliongozwa na Kwaya ya Kanisa ambao walimtukuza Mungu kwa nyimbo za sifa na shukrani tangu vipindi vya asubuhi mpaka jioni. Pia ilikuwa ni siku ambayo Kwaya ya Kanisa ilitambulisha rasmi albam yake iliyorekodiwa ndani ya mwaka huu 2014 iitwayo ''MTUKUZENI".


    Kwaya ya Kanisa ikiimba wakati wa Ibada asubuhi
     Ruth Chaulo akihudumu katika Shule ya Sabato na
    Mwalimu Daniel Sempambo akiiimba pamoja na Kwaya.

     Wanakwaya wakiimba wakati wa kipindi cha mchana.


    Kwaya hii ya kanisa la waadventista wasabato Ilala imepata kuhudumu katika siku maalum ya kuweka wakfu kanisa la waadventista wasabato Kimara terehe 23/11/2014 katika viwanja vya kanisa hilo.
    Kwaya hii imepata kutoa huduma ya uimbaji kama kwaya aliyoalikwa siku hii na kuimba nyimbo kama;-"Mungu wetu twamshukuru sana" huu ukiwa ni wimbo maalum,hivi nilivyo mimi,Yesu aliniita njoo na mwisho kwaya hii ikapata kuimba wimbo wa pamoja na kwaya ya Kimara ambao unaitwa "Naweka hazina yangu Mbinguni"
    PICNIC YA VIJANA

    Kiongozi wa Vijana(AY) Anthony Mwainyekule akitoa somo fupi kuhusu vijana.

    Anthony Mwainyekule akiongoza vijana katika mazoezi ya viungo

     Baadhi ya vijana wakifurahia ukuu wa Mungu kupitia mchanga wa bahari

     Peter Joseph na Rose Joseph wakibuni taswira ya msalaba

    .mslaba umekamilika sasa...

    STAND UP FOR JESUS

  • You might also like