Mwimbaji wa Sauti ya kwanza wa Ambassadors of Christ ya Rwanda Humure
Rebecca amechumbiwa na Mwimbaji na Kiongozi wa kundi la Voices of
Victory la jijini Dar es salaam,Warren Bright,sherehe fupi ya uchumba
ilifanyika nyumbani kwa wazazi wa Warren Bright,Kunduchi jijini Dar es
salaam Agosti 17,2013 na ilihudhuriwa na baadhi ya waimbaji mbalimbali
wa nyimbo za injili nchini Tanzania na mwimbaji wa kiume wa Ambassadors
of Christ, Nelson Manzi.
Warren ambaye ameweka picha za tukio hilo katika wasifu wake wa facebook
amesema harusi yao inatarajiwa kufanyika hivi karibuni. Warren pia
amekuwa mmoja wa waimbaji wa kwaya hiyo ya Ambassadors of Christ ambapo
amekuwa akienda nchini Rwanda kuimba na kwaya hiyo pamoja na kufanya
baadhi ya ziara pamoja na kwaya hiyo.
Warren wa pili kutoka kushoto akiimba pamoja na waimbaji wa Ambassadors walipotembelea nchini Kenya mapema mwaka huu. Habari kwa hisani ya networkedblogs, Picha zote mali ya Warren Bright. GK inawatakia kila la kheri